Majaliwa aahirisha kugombea Ruangwa 2025

Majaliwa aahirisha kugombea Ruangwa 2025

#1

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kassim Majaliwa, hatogombea tena Ubunge wa Ruangwa katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 kama alivyoahidi mara kadhaa ikiwemo juzi akiwa Bungeni, chanzo cha kuaminika kimeiambia AyoTV.



Waziri Mkuu Majaliwa ambaye amekuwa Mbunge wa Ruangwa kwa miaka 15 kuanzia mwaka 2010, aliteuliwa kwa mara ya kwanza kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2015 katika awamu ya tano chini ya Hayati Dr. John Pombe Magufuli na kisha kuaminiwa na awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kuendelea kuhudumu katika nafasi hiyohiyo baada ya Rais Magufuli kufariki.

 Via:MillardAyoUPDATES

Related Discussions

REPLY HAPA


image quote pre code