Mapigano Syria Waliokufa wafikia watu 500

Mapigano Syria Waliokufa wafikia watu 500

#1

Idadi ya vifo vilivyotokana na ghasia kusini mwa mji wa Sweida nchini Syria inaendelea kuongezeka na sasa imepindukia 500 kufuatia mapigano makali yaliyozuka Julai 13.



Idadi ya vifo vilivyotokana na ghasia kusini mwa mji wa Sweida nchini Syria inaendelea kuongezeka na sasa imepindukia 500 kufuatia mapigano makali yaliyozuka Julai 13.

Shirika linalofuatilia haki za binadamu la Syria lenye makao yake makuu Uingereza limerekodi vifo vya raia 83 wa jamii ya Druze katika mitaa ya mji wa Sweida na viunga vyake vya karibu huku likisema vikosi vya serikali ndio vimehusika na mauaji hayo.

Katika ripoti nyingine, shirika hilo limesema watu watatu wa jamii ya Bedui akiwemo mwanamke, mtoto na mwanaume wameuawa na wapiganaji wa Druze mjini humo.Vikosi vya Syria vyaanza kujiondoa kutoka mjini Sweida

Hadi kufikia jana vikosi vya serikali ya Syria kwa kiasi kikubwa vilijiondoa katika jimbo la Sweida baada ya siku kadhaa za mapigano na wanamgambo wanaohusishwa na jamii ya watu walio wachache wa Druze.

Via:Dw.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code