Maumivu ya magoti,chanzo,dalili na tiba

Maumivu ya magoti,chanzo,dalili na tiba

#1

Tatizo hili huweza kutokea kwa kila mtu bila kujali umri wala jinsia yake. na zipo sababu mbali mbali ambazo huweza kuhusishwa moja kwa moja na maumivu makali ya magoti.



SABABU ZA MAUMIVU YA MAGOTI NI PAMOJA NA;

- Mtu kupata ajali,kuanguka na kuumia kwenye goti au magoti n.k

- Mtu kuwa na matatizo ya mifupa

- Maambukizi ya magonjwa mbali mbali

- Mtu kukaa kwa muda mrefu

- Kutokufanya mazoezi ya mwili pamoja na viungo

- Mtu kuwa na historia ya kuumia goti au magoti hapo nyuma

- Mtu kuwa na matatizo ya Gauti

- Kuwa na shida ya unene au uzito kupita kiasi

DALILI ZA TATIZO HILI LA MAUMIVU MAKALI KWENYE MAGOTI

✓ Sehemu ya goti kubadilika rangi na kuwa nyekundu kuliko kawaida

✓ Kupata maumivu makali ya goti

✓ Goti kukaza sana 

✓ Kushindwa kunyoosha mguu

✓ Kushindwa kutembea 

MATIBABU YA TATIZO HILI

Matibabu ya tatizo hili hutegemea chanzo chake,hivo mgonjwa atapewa dawa za kutuliza maumivu pamoja na matibabu mengine kulingana na chanzo cha tatizo kama vile; Kutibu matatizo ya mifupa,gauti, majeraha,kuvunjika N.k

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU AU TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code