Tiba ya kwanza ya malaria kwa watoto yaidhinishwa kutumika

Tiba ya kwanza ya malaria kwa watoto yaidhinishwa kutumika

#1

Tiba ya kwanza ya malaria inayofaa kwa watoto wachanga na wadogo imeidhinishwa.



Inatarajiwa kuanza kutumika katika nchi za Afrika ndani ya wiki kadhaa.

Hadi kufikia sasa hakuna dawa za malaria zilizoidhinishwa hasa kwa watoto.

Badala yake wamekuwa wakitibiwa kwa matoleo yaliyotengenezwa kwa ajili ya watoto wakubwa jambo ambalo linaleta hatari ya kuzidisha dozi.

Vifo nusu milioni mnamo 2023

Mnamo mwaka 2023 - mwaka ambao takwimu za hivi karibuni zinapatikana - ugonjwa wa malaria ulihusishwa na karibu vifo 597,000.

Takriban vifo vyote vilitokea barani Afrika, na karibu robo tatu yao walikuwa watoto chini ya miaka mitano.

Matibabu ya malaria kwa watoto yapo lakini hadi sasa, hakukuwa na matibabu mahsusi kwa watoto wachanga zaidi na wadogo, ambao wana uzito wa chini ya 4.5kg au karibu 10lb.

Badala yake wametibiwa kwa dawa zilizotengenezwa kwa ajili ya watoto wakubwa.

Lakini hiyo ni hatari, kwani dozi kwa watoto hawa wakubwa huenda isiwe salama kwa Watoto wadogo, ambao uwezo wa ini bado unaendelea kukua na ambao miili yao huchakata dawa kwa njia tofauti.

Wataalamu wanasema hii imesababisha kile kinachoelezwa kuwa "pengo la kimatibabu".

Sasa dawa mpya, iliyotengenezwa na kampuni ya dawa ya Novartis, imeidhinishwa na mamlaka ya Uswizi na kuna uwezekano wa kusambazwa katika mikoa na nchi zilizo na viwango vya juu vya malaria ndani ya wiki kadhaa.

Novartis inapanga kuitambulisha kwa misingi isiyo ya faida.

Related Discussions

REPLY HAPA


image quote pre code