Afyaclass Bongo Social MAFURIKO:Zaidi ya watu 89,000 wamehamishwa nchini Pakistan.

MAFURIKO:Zaidi ya watu 89,000 wamehamishwa nchini Pakistan.



Pakistan imewahamisha maelfu ya watu na kuwapeleka maeneo salama baada ya nchi jirani ya India kufunguwa mabwawa yake yaliyofurika pamoja na mito na kuyaachia maji kumiminika kuelekea katika mikoa ya mpakani iliyoko nyanda za chini.

Pakistan imechukuwa hatua ya kuwahamisha raia wake kwenye maeneo hayo baada ya serikali ya mjini New Delhi kuifahamisha juu ya uwezekano wa kutokea mafuriko kwenye maeneo hayo ya mpakani na nchi hiyo.

Mawasiliano hayo ya kidiplomasia kati ya nchi hizo mbili zenye mivutano yamefanyika kwa mara ya kwanza ndani ya kipindi cha miezi kadhaa. Zaidi ya watu 89,000 wamehamishwa kutoka kwenye maeneo ya mpakani nchini Pakistan.

You, Mehreen and others

WEKA MAONI HAPA(Reply)

Notification
Karibu Afyaclass Bongo Social Jukwaa linalojadili mambo mbali mbali ikiwemo afya,Magonjwa na Updates Zote,Tembelea hapa kila Siku,Pia Share Maoni yako kwenye jukwaa hili Afyaclass Bongo Social ASANTE.
UNDERSTOOD