Marekani imesitisha uchakataji wa Maombi ya Visa nchini Zimbabwe

Marekani imesitisha uchakataji wa Maombi ya Visa nchini Zimbabwe

#1

Marekani imesitisha uchakataji wa Maombi ya Visa nchini Zimbabwe

Marekani imesitisha uchakataji wa Maombi ya Visa nchini Zimbabwe mpaka hapo taarifa kwa kina itakapo tolewa ambapo Ubalozi wa Marekani mjini Harare umesema uamuzi huo umetokana na wasiwasi fulani dhidi ya Zimbabwe japo wasiwasi haujawekwa bayana.

Usitishaji wa maombi mapya ya Visa umeanza tangu agost 7 kwa huduma zote za Visa Isipokuwa zile za Kidiplomasia na kiofisi zitaendelea kutolewa ambapo Ubalozi wa Marekani pia umeeleza kuwa hatua hiyo sio marufuku ya kusafiri kwenda Marekani na wale ambao walishapatiwa Visa zitaendelea kuwa halali lakini hakuna maombi mapya ya Visa yatakayo shughulikiwa kwa sasa.

Kisitishwa huko kwa Utoaji wa Visa kwa wananchama kumekuja baada ya masharti ya awali ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani linalolenga kudhibiti tatizo la watu kuzidisha muda wa ukaaji kinyume na masharti ya Visa ambapo ripoti zinaonesha kuwa kiwango cha kuzidisha muda wa ukaaji nchini Marekani kwa raia wa Zimbabwe kilifikia asilimia 10.57 mwaka 2023.

Hata hivyo kwa upande mwingine wa nchi za Afrika kama vile Zambia na Malawi raia wake watalazimika kuweka dhamana ya hadi dola 15,000 kwa aina fulani za viza za wageni ili waweze kuzingatia mashart ya Kuishi Marekani.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code