Mpango kamili wa Lishe kwa Mtu mwenye HIV alafu kakonda sana

Mpango kamili wa Lishe kwa Mtu mwenye HIV alafu kakonda sana

#1

Mpango kamili wa Lishe kwa Mtu mwenye HIV alafu kakonda sana



Mtu mwenye HIV ambaye amekonda sana anahitaji mpango kamili wa lishe na uangalizi wa karibu ili:

  • Kupata nguvu
  • Kuongeza uzito kwa afya
  • Kuimarisha kinga ya mwili
  • Kupambana na maambukizi mengine

Nitakupa full package ya baadhi ya Vitu vya Kufanya:

1. MISINGI YA LISHE KWA MWENYE HIV ALIYEKONDA

a) ALE VYAKULA VINAVYOTOA NGUVU (KABOHIDRETI)

b) ALE VYAKULA VYA PROTINI

Hizi husaidia kutengeneza misuli na kuimarisha kinga:

  • Nyama (kuku, samaki, maini)
  • Maziwa na mtindi
  • Maharage, kunde, choroko, dengu
  • Mayai
  • Njugu na karanga (hazikaangwi sana)

c) MATUNDA NA MBOGAMBOGA (vitamini na madini)

  • Mchicha, matembele, sukuma wiki, spinach
  • Karoti, hoho, nyanya, pilipili hoho
  • Matunda: embe, ndizi, papai, nanasi, apple, machungwa, zabibu

d) MAFUTA MAZURI KIAFYA (kuongeza kalori)

  • Tumia mafuta ya alizeti, karanga, nazi au mzeituni kwa kiasi
  • Ongeza maziwa ya nazi kwenye uji au wali
  • Tumia karanga, parachichi mara kwa mara

 2. JINSI YA KULA KWA MTU MWENYE HIV ALIYEKONDA

  • Ale milo midogo mara 5 hadi 6 kwa siku (milo 3 mikuu + snacks 2-3)
  • Asilimia kubwa ya chakula iwe ya kuongeza uzito (protini + mafuta)
  • Anywe maji mengi (angalau lita 2 kwa siku)

3. SUPLIMENTS ZINAZOWEZA SAIDIA

  • Multivitamin (kila siku) – kusaidia upatikanaji wa virutubisho
  • Probiotic au mtindi wa asili – kwa afya ya tumbo
  • Plumpy’Nut au lishe za hospitali kama F-75 / F-100 (kwa waliokonda sana sana)
  • Lishe ya unga wa lishe nyumbani (mtama + karanga + maziwa ya unga + soya)

4. VITU VYA KUZINGATIA

a) Matibabu

  • Awe anatumia dawa za ARV kila siku bila kuruka
  • Adhibiti magonjwa nyemelezi (kifua, kuharisha, fangasi nk)
  • Afuatiliwe kliniki mara kwa mara – uzito na hali ya damu

b) Epuka

  • Vyakula vichafu au visivyopikwa vizuri (kuharisha hupunguza uzito zaidi)
  • Acha kabsa Unywaji wa pombe/sigara – hupunguza kinga na hamu ya kula
  • Msongo wa mawazo (upunguze kwa mazungumzo, sala, au ushauri)

5. MFANO WA RATIBA YA CHAKULA KWA SIKU

Wakati Chakula
Asubuhi Uji wa lishe (mtama + karanga + maziwa ya unga), mayai 2, parachichi nusu
Saa 4 Tunda (ndizi 2 au embe 1), karanga mkononi
Mchana Ugali wa dona, mboga za majani, maharage, kipande cha samaki, kikombe cha mtindi
Saa 10 Juice ya asili + mkate na siagi
Usiku Wali wa nazi, maharage/mishikaki ya nyama, mboga mbichi (saladi)
Kabla kulala Maziwa ya moto kikombe + ndizi

📌 MUHIMU:

Ikiwezekana aonane na daktari wa lishe au clinic ya HIV kwa mpango wa kina na ufuatiliaji wa uzito kila wiki.

Consultation ya Afya Moja kwa Moja

Mimi ni Dr. Ombeni Mkumbwa. Nakupa ushauri wa kitaalamu kuhusu tatizo lolote la kiafya kwa siri, haraka na uhakika.

WhatsApp

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code