Mpango kamili wa Lishe kwa Mtu mwenye HIV alafu kakonda sana

Mpango kamili wa Lishe kwa Mtu mwenye HIV alafu kakonda sana

#1

Mpango kamili wa Lishe kwa Mtu mwenye HIV alafu kakonda sana



Mtu mwenye HIV ambaye amekonda sana anahitaji mpango kamili wa lishe na uangalizi wa karibu ili:

  • Kupata nguvu
  • Kuongeza uzito kwa afya
  • Kuimarisha kinga ya mwili
  • Kupambana na maambukizi mengine

Nitakupa full package ya baadhi ya Vitu vya Kufanya:

1. MISINGI YA LISHE KWA MWENYE HIV ALIYEKONDA

a) ALE VYAKULA VINAVYOTOA NGUVU (KABOHIDRETI)

b) ALE VYAKULA VYA PROTINI

Hizi husaidia kutengeneza misuli na kuimarisha kinga:

  • Nyama (kuku, samaki, maini)
  • Maziwa na mtindi
  • Maharage, kunde, choroko, dengu
  • Mayai
  • Njugu na karanga (hazikaangwi sana)

c) MATUNDA NA MBOGAMBOGA (vitamini na madini)

  • Mchicha, matembele, sukuma wiki, spinach
  • Karoti, hoho, nyanya, pilipili hoho
  • Matunda: embe, ndizi, papai, nanasi, apple, machungwa, zabibu

d) MAFUTA MAZURI KIAFYA (kuongeza kalori)

  • Tumia mafuta ya alizeti, karanga, nazi au mzeituni kwa kiasi
  • Ongeza maziwa ya nazi kwenye uji au wali
  • Tumia karanga, parachichi mara kwa mara

 2. JINSI YA KULA KWA MTU MWENYE HIV ALIYEKONDA

  • Ale milo midogo mara 5 hadi 6 kwa siku (milo 3 mikuu + snacks 2-3)
  • Asilimia kubwa ya chakula iwe ya kuongeza uzito (protini + mafuta)
  • Anywe maji mengi (angalau lita 2 kwa siku)

3. SUPLIMENTS ZINAZOWEZA SAIDIA

  • Multivitamin (kila siku) – kusaidia upatikanaji wa virutubisho
  • Probiotic au mtindi wa asili – kwa afya ya tumbo
  • Plumpy’Nut au lishe za hospitali kama F-75 / F-100 (kwa waliokonda sana sana)
  • Lishe ya unga wa lishe nyumbani (mtama + karanga + maziwa ya unga + soya)

4. VITU VYA KUZINGATIA

a) Matibabu

  • Awe anatumia dawa za ARV kila siku bila kuruka
  • Adhibiti magonjwa nyemelezi (kifua, kuharisha, fangasi nk)
  • Afuatiliwe kliniki mara kwa mara – uzito na hali ya damu

b) Epuka

  • Vyakula vichafu au visivyopikwa vizuri (kuharisha hupunguza uzito zaidi)
  • Acha kabsa Unywaji wa pombe/sigara – hupunguza kinga na hamu ya kula
  • Msongo wa mawazo (upunguze kwa mazungumzo, sala, au ushauri)

5. MFANO WA RATIBA YA CHAKULA KWA SIKU

Wakati Chakula
Asubuhi Uji wa lishe (mtama + karanga + maziwa ya unga), mayai 2, parachichi nusu
Saa 4 Tunda (ndizi 2 au embe 1), karanga mkononi
Mchana Ugali wa dona, mboga za majani, maharage, kipande cha samaki, kikombe cha mtindi
Saa 10 Juice ya asili + mkate na siagi
Usiku Wali wa nazi, maharage/mishikaki ya nyama, mboga mbichi (saladi)
Kabla kulala Maziwa ya moto kikombe + ndizi

📌 MUHIMU:

Ikiwezekana aonane na daktari wa lishe au clinic ya HIV kwa mpango wa kina na ufuatiliaji wa uzito kila wiki.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code