Mtoto 'mkongwe' zaidi duniani azaliwa baada ya miaka 30
Familia moja nchini Marekani imejaaliwa kupata mtoto wa kiume aliyezaliwa kutokana na kiini tete kilichogandishwa kwa zaidi ya miaka 30, na kuandikisha historia mpya duniani.
Lindsey, 35, na Tim Pierce, 34, walimpata mtoto wao wa kiume, Thaddeus Daniel Pierce, siku ya Jumamosi. Pierce aliiambia mtandao wa MIT Technology Review kwamba familia yake ilifananisha tukio hilo na " kitu kama filamu ya kisayansi ".
Inaaminika kuwa huo ndio muda mrefu zaidi ambao kiini tete kimewahi kugandishwa kabla ya mimba kutungishwa na hatimaye mtoto kuzaliwa. Rokodi ya awali inashikiliwa na pacha waliozaliwa 2022 kutokana na kiini tete kilichogandishwa mwaka 1992.
Pierce na mpenzi wake walijaribu kupata mtoto kwa miaka saba bila mafanikio kabla ya kuamua kuasili kiini tete cha Linda Archerd, 62, kilichotengenezwa kutokana yai lake na manii ya mume wake wa zamani mwaka 1994, na mimba kutungishwa kwa njia ya upandikizaji inayofahamika kwa kimombo In Vitro Fertilization (IVF).
image quote pre code