Mungu hulituma Neno lake ili tupone, na Siku ya Leo anakuuliza;Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda Bwana?
Kama hakuna,basi hata hicho unachopitia,au hicho unachokiona kigumu sana kwako,Yeye anaweza kukusaidia.
Ujumbe huu,unakukumbusha kwamba,Mungu anaweza kila kitu,Mpe nafasi akusaidie,Peke yako hutaweza.
Ukisoma habari za Sara,kwenye kitabu cha Mwanzo18,Mungu alimletea neno la Kumsaidia ili apate ujauzito,akawa halipokei,Mungu akamkumbusha,kwani kuna neno gani gumu la kumshinda Bwana; Hii ilimfanya kupandisha imani yake ya kupokea:Ndipo akapandisha imani yake na kupokea muujiza wake. Biblia inasema kwa Imani hata Sara mwenyewe alipokea uwezo wa kuwa na Mimba,ingawa ni mzee,hata Desturi ya wanawake Imekoma Kabsa.
Na wewe haijalishi ni kitu gani unaona kigumu sana kwako,Pandisha Imani yako kwa Mungu,upate majibu ya tatizo lako. Mungu anaweza kila kitu.....!!!!
"Mwanzo 18:14 Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda Bwana? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume".
image quote pre code