Sasa CHATGPT kuacha kushauri Wapenzi waachane

Sasa CHATGPT kuacha kushauri Wapenzi waachane

#1

Kampuni ya OpenAI imetangaza kuwa programu yake ya mazungumzo, ChatGPT, haitatoa tena majibu ya moja kwa moja kwa watumiaji wanaotaka ushauri wa kuachana na wapenzi wao.



Badala yake, ChatGPT itawaongoza watumiaji kutafakari kwa kina kwa kuwasaidia kupima faida na hasara kabla ya kufanya uamuzi .

OpenAI imesema hatua hiyo inalenga kulinda afya ya akili ya watumiaji, hasa wanapopitia changamoto binafsi. Pia, kampuni hiyo imeanza kushirikiana na wataalamu zaidi ya 90 wa afya ya akili kutoka nchi 30 ili kuhakikisha majibu yanayotolewa ni salama na yanayojali hali ya mtumiaji.

Mabadiliko mengine ni pamoja na ujumbe wa kuwakumbusha watumiaji kuchukua mapumziko wakati wa mazungumzo marefu ili kuepuka utegemezi kupita kiasi.

Kwa sasa, ChatGPT inatumiwa na zaidi ya watu milioni 700 kwa mwezi.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code