Simba kuzindua jezi mpya kwa njia ya Kipekee August 27 2025

Simba kuzindua jezi mpya kwa njia ya Kipekee August 27 2025

#1

Simba kuzindua jezi mpya kwa njia ya Kipekee August 27 2025



Mkuu wa Idara ya Habari ya Simba SC Ahmed Ally leo ametangaza rasmi kuwa watazindua jezi zao mpya kwa mara ya kwanza jezi katika njia ya kipekee August 27 2025 katika ukumbi wa Super Dome Masaki.

Upekee wa tukio hili ni kuwa kwa mara ya kwanza wataruhusu shabiki yoyote kuhudhuria tukio kwa Kingilio cha Tsh 250,000/= na unapewa jezi za aina zote tatu bure.

“Yeyote ambaye atahitaji kuhudhuria tukio hili la uzinduzi wa jezi na kuwa mtu wa kwanza kuona jezi ya Simba msimu huu atalipa Tsh. 250,000. Akishalipa hiyo fedha yote ambayo atapata ndani ya ukumbi ni juu yetu na baada ya hapo atapewa jezi zote tatu za msimu huu. Vyote hivyo atakabidhiwa hapo hapo ukumbini”- Semaji Ahmed Ally.

Huu ndio msimu wa kwanza wa jezi za Simba SC kuzalishwa na mzabuni mpya Jayrutty kwa kushirikiana na Diadora ambayo ni Kampuni ya Kiitaliano na tayari ilishatoa jezi za mazoezi za Simba SC.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code