Katika Safari ya kuelekea Kanani yako(Mahali ambapo Mungu kakupangia) lazima uwe Hodari na Moyo wa Ushujaa,Hii ina maana lazima Upinzani,Vikwanzo,Majaribu,Kutishwa,kukatishwa tamaa n.k. Vitakuwepo.
Haimaanishi kwa Vile Mungu kakupa,hutapata kikwazo chochote,na haimaanishi Mungu kuwa Upande wako hataibuka Mjaribu.
Kitakachotokea ni kwamba; Mungu akiwa upande wako,atapigana na kila Adui anayesimama mbele yako,atawaondoa mhiti,Mperizi,Myebusi, na kila aina ya kikwazo mbele yako. Wewe unachotakiwa ni kuimarisha Imani yako kwake.
Yoshua wakati Mungu anampa jukumu la kupeleka Wana wa Israel Kanani, Ingawa Mungu alikuwa Pamoja naye, anamwambia;Uwe Hodari na Moyo wa Ushujaa.
Soma:Yoshua 1:6 "Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakayewarithisha watu hawa nchi hii niliyowaapia baba zao ya kwamba nitawapa".
Hata kama kuna kanani yako Mungu amekupa,Adui watainuka tu. Unachotakiwa ni kuwa hodari na Moyo wa Ushujaa,Utafika Kanani yako.
image quote pre code