Hedhi ya muda mrefu au hedhi mfululizo chanzo chake

Hedhi ya muda mrefu au hedhi mfululizo chanzo chake

#1

Hedhi ya muda mrefu au hedhi mfululizo (inayodumu zaidi ya siku 7 au kurudi mara kwa mara bila kupumzika) mara nyingi ni ishara ya tatizo la kiafya. Sababu zake kuu ni:



Vyanzo vya hedhi ya muda mrefu/mfululizo

1. Mabadiliko ya homoni, au Tatizo la hormone imbalance

  • Upungufu wa homoni ya progesterone au ongezeko la estrogen huchangia ukuta wa mfuko wa uzazi kukua kupita kiasi na kutoka damu nyingi.
  • Mara nyingi hutokea kwa wasichana walio katika balehe au wanawake wanaokaribia kukoma hedhi.

2. Uvimbe na ukuaji usio wa kawaida

Hapa tunazungumzia matatizo mbali mbali kwenye kizazi kama vile;

  • Tatizo la Fibroids (uvimbe kwenye mfuko wa uzazi).
  • Polyps za kwenye kizazi.
  • Saratani ya mfuko wa uzazi au shingo ya kizazi.n.k

3. Magonjwa ya damu na matatizo ya kuganda kwa damu

Upungufu wa chembe sahani (platelets).

Magonjwa ya kurithi ya damu kama hemophilia.n.k. huweza pia kuchangia hali hii

4. Matumizi ya baadhi ya dawa,Mfano;

Vidonge vya uzazi wa mpango visivyotumika ipasavyo.

Dawa za kupunguza damu (anticoagulants).n.k.

5. Madhara ya baadhi ya Njia za uzazi wa mpango,kama vile;

  • Vidonge
  • Sindano n.k.

6. Maambukizi ya magonjwa mbali mbali

Mfano; Maambukizi ya bacteria kwenye via vya uzazi vya Mwanamke au (PID).n.k.

7. Sababu nyingine

Msongo wa mawazo, uzito mkubwa kupita kiasi au kupungua ghafla, matatizo ya tezi (thyroid disorders). n.k.

🔔 Tahadhari:
Hedhi ya muda mrefu au mfululizo huweza kusababisha upungufu wa damu (anemia) kwa haraka.

Ikiwa damu inatoka kwa wingi sana (unabadili pedi kila chini ya saa 1–2), unaona damu yenye mabonge makubwa, au unahisi kizunguzungu na kuchoka sana, unapaswa kumuona daktari haraka.

KWA USHAURI ZAIDI,ELIMU NA TIBA TUWASILIANE KWA NAMBA +255758286584.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code