Imani ina nguvu ya Kufungua Lango la Uponyaji kwako,bila kujali aina ya Ugonjwa ulionao,wala Muda wa Ugonjwa unaokusumbua. Soma kisa hiki...
Tazama, mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, amehangaika kila mahali,kaenda kwa matabibu wengi,katumia vyote alivyokuwa navyo asipate kupona ugonjwa wake.
Akaenda kwa YESU kwa Imani akisema Nikiyagusa mavazi yake tu, nitapona.
Mathayo 9:22 "Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu; IMANI YAKO IMEKUPONYA. Yule mwanamke akapona tangu saa ile".
Marko 5:29 "Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, naye akafahamu mwilini mwake kwamba amepona msiba ule".
Soma "Mathayo 9:20–22,Marko 5:25–34"
Na wewe Nenda kwa Yesu kwa Imani,Peleka Ugonjwa wako kwake,Utapokea Uponyaji.....
image quote pre code