Kuongezeka kwa idadi ya Simba Nchini India yawa tishio

Kuongezeka kwa idadi ya Simba Nchini India yawa tishio

#1

Kuongezeka kwa idadi ya Simba Nchini India yawa tishio

Japokuwa kitendo cha kuongezeka kwa idadi ya Simba Nchini India kinaonekana kama ni mafanikio kwenye sekta ya uhifadhi, kwa upande mwingine kitendo hicho kinaonekana kuwa tishio kwa maisha ya Binadamu na Mifugo katika Jimbo la Gujarat, Magharibi mwa Nchi hiyo.

Simba hao wamekuwa wakiua Binadamu pamoja na Mifugo ambapo tukio la hivi karibuni linamhusu Mtoto wa miaka mitano aliyeuawa na Simba wakati akicheza na Kaka zake kwenye shamba lililo karibu na nyumba yao ambapo Baba yake amesema Simba huyo alitokea ghafla na kumbeba Mtoto huyo licha ya Familia yake kurusha mawe na fimbo kujaribu kumuokoa na kisha baada ya muda mwili wa Mtoto huyo ulipatikana Msituni.

Mtoto huyo ni mmoja wa Watu saba waliouawa na Simba kati ya Juni 2024 na Juni 2025 ambapo katika kipindi cha miaka mitano iliyopita zaidi ya Watu 20 wamepoteza maisha kwa mashambulizi ya Simba huku visa vya kushambuliwa kwa Mifugo vikiongezeka maradufu.

Simba wa Asia ambao ni wadogo kidogo kuliko Simba wa Afrika hutambulika kwa manyoya meusi mazito na mikunjo ya ngozi tumboni mwao ambapo inaelezwa kuwa waliwahi kuishi katika maeneo ya Mashariki ya Kati na Asia lakini sasa Jimbo la Gujarat ndilo pekee Duniani lenye Simba pori hao.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code