Tumia maombi ya Shukurani ili kuingia kwenye Uwepo wa Mungu

Tumia maombi ya Shukurani ili kuingia kwenye Uwepo wa Mungu

#1

Tumia maombi ya Shukurani ili kuingia kwenye Uwepo wa Mungu

Zaburi 100:4 "Ingieni malangoni mwake kwa kushukuru; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake".

Aina hii ya maombi;

•Humfanya Mungu akukaribie na kukusaidia

•Huleta Ongezeko,Mfano Yesu alitumia maombi ya Kushukuru;Mikate na Samaki wakaongezeka sana(Soma yohana 6:11)

Yohana 6:9-11

Mstari wa 9"Yupo hapa mtoto, yuna mikate mitano ya shayiri na samaki wawili, lakini hivi ni nini kwa watu wengi kama hawa?

Mstari wa 10 "Yesu akasema, Waketisheni watu. Na mahali pale palikuwa na majani tele. Basi watu waume wakaketi, wapata elfu tano jumla yao.

Mstari wa 11 "Basi Yesu akaitwaa ile mikate, akashukuru, akawagawia walioketi; na kadhalika katika wale samaki kwa kadiri walivyotaka.

•Ni Silaha dhidi ya manung'uniko:Nenda mbele za Mungu kwa Kumshukuru hata kama kuna mambo hajafanya kama vile ulivyotaka, Hali ya kunung'unika itaondoka ndani yako,Imani yako kwake itaongezeka Na Mungu atajibu na haja zako ulizonazo.

Tazama Full Video Hapa:

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code