Kimbunga Melissa ni tishio katika eneo la Carribea,Watoto millioni 1.6 hatarini
Wakati Kimbunga Melissa kikitarajiwa kuleta mvua kubwa na upepo mkali katika eneo la Carribea, takriban watoto milioni 1.6 wako hatarini, huku familia katika nchi za Jamaica, Haiti na visiwa jirani zikijiandaa kwa mafuriko, maporomoko ya ardhi na uharibifu mkubwa kwa mujibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF.
Kwa sasa kimbunga hicho kipo katika ukali wa daraja la 4 na kinajongea taratibu katika Bahari ya Cariibea, huku kikitarajiwa kuimarika hadi daraja la 5, kikiwa na upepo unaoendelea wa angalau maili 157 kwa saa ambazo ni takriban km 252 kwa saa.
Nchi mbalimbali katika eneo hilo, ikiwemo Jamaica, Haiti, Cuba na Jamhuri ya Dominika, zinatarajiwa kukabili siku kadhaa za hali mbaya ya hewa, huku wakiogopa kwamba miundombinu inaweza kushindwa kuhimili na huduma muhimu kuathirika.





.jpg)


image quote pre code