Maji machafu ni chanzo cha Ugonjwa wa Kipindupindu

Maji machafu ni chanzo cha Ugonjwa wa Kipindupindu

#1

Maji machafu au yasiyochemshwa yanaweza kusababisha kipindupindu. Hii ni kwa sababu vimelea vya Vibrio cholerae (bakteria wanaosababisha kipindupindu) huishi na kusambaa kupitia maji na chakula kilichochafuliwa na kinyesi cha binadamu.

Maji machafu huleta kipindupindu kwa njia hizi:

-Kunywa maji machafu yenye vijidudu vya kipindupindu.

-Kutumia maji machafu kupikia au kuosha vyombo.

-Kuoga au kusafisha chakula kwa maji yasiyo safi.

-Kuchanganyika na kinyesi kilichoingia kwenye vyanzo vya maji.

Njia za kujikinga:

1. Chemsha maji kabla ya kunywa.

2. Tumia vidonge vya kutibu maji (water guard/chlorine).

3. Hifadhi maji kwenye chombo safi kilichofunikwa.

4. Osha mikono kwa sabuni kabla ya kula na baada ya choo.

5. Epuka kula chakula kilichoandaliwa sehemu zisizo safi.

Consultation ya Afya Moja kwa Moja

Mimi ni Dr. Ombeni Mkumbwa. Nakupa ushauri wa kitaalamu kuhusu tatizo lolote la kiafya kwa siri, haraka na uhakika.

WhatsApp

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code