Chanjo mpya za TB zina uwezo wa kuokoa maisha ya mamilioni ya watu kwa haraka 'WHO'

Chanjo mpya za TB zina uwezo wa kuokoa maisha ya mamilioni ya watu kwa haraka 'WHO'

#1

Ripoti:WHO yahimiza hatua thabiti kuhakikisha upatikanaji sawa wa chanjo mpya za TB

WHO inasisitiza umuhimu wa utafiti kuhusu ugonjwa wa Kifua kikuu hasa kile kilicho sugu dhidi ya dawa.

Shirika la Afya Duniani (WHO) limezindua ripoti mpya leo pembezoni mwa Mkutano wa Mawaziri wa Afya wa G20 uliofanyika Limpopo, Afrika Kusini, likitoa wito kwa hatua thabiti za kifedha na upatikanaji ili kuhakikisha chanjo mpya za kifua kikuu  (TB) zinawafikia vijana balehe na watu wazima katika nchi zenye mzigo mkubwa wa ugonjwa huo.

Ripoti hiyo, yenye kichwa, “kuchochea suluhisho kwa upatikanaji sawa duniani na ufadhili endelevu wa chanjo mpya za kifua kikuu kwa watu wazima na vijana,” imetoa uchambuzi wa kwanza wa aina yake kuhusu vikwazo vinavyotarajiwa, vizuizi, na mienendo ya soko ambayo inaweza kuathiri upatikanaji wa wakati, usawa, na endelevu wa chanjo mpya za TB.

“Chanjo mpya za TB zina uwezo wa kuokoa maisha ya mamilioni ya watu kwa haraka na kubadilisha mwelekeo wa janga hili, kwa kutumia nguvu ya sayansi, ushirikiano na fedha, tunaweza kufanikisha maono yetu ya pamoja ya kutokomeza kifua kikuu.”  amesema Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus, Mkurugenzi Mkuu wa WHO.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code