Mshambuliaji wa Yanga SC, Clement Mzize, ameshinda tuzo ya Goli Bora la Mwaka (CAF Goal of the Season 2025) katika Tuzo za Shirikisho la Soka Afrika (CAF) 2025.
Mzize alithibitisha ubora wake baada ya kufunga goli la shuti la mbali wakati wa mchezo dhidi ya TP Mazembe, katika hatua ya makundi ya Michuano ya Klabu Bingwa Afrika msimu uliopita.
Goli hilo limechaguliwa kuwa bora zaidi kutokana na ubora wa kiufundi, ufanisi na umuhimu wake katika michezo ya mashindano ya klabu bingwa barani Afrika, na limeipa Mzize heshima kubwa katika soka la kikanda.









image quote pre code