Chanjo Gaza: WHO, UNICEF na UNRWA waanza uchanjaji zaidi ya watoto 44,000
Mashirika ya Umoja wa Mataifa WHO, UNICEF na UNRWA wameanzisha kampeni ya pamoja ya Uchanjaji watoto waliokosa huduma muhimu za kuokoa maisha kutokana na miaka miwili ya machafuko katika Ukanda wa Gaza umeanza kutekelezwa na mashirika matatu ya Umoja wa Mataifa, lile la afya duniani, la kuhudumia watoto UNICEF na la kusaidia wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA.
Kampeni hii inayowalenga watoto kuanzia siku moja hadi miaka mitatu, imeanza majuzi tarehe 10 mwezi huu wa Novemba na itaendelea hadi tarehe 18 Novemba. Utoaji wa huduma hizi muhimu za afya kwa maelfu ya watoto unategemea kuheshimiwa kwa usitishaji mapigano kuhakikisha familia, wataalamu wa afya na wahudumu wa kibinadamu wanaweza kufika katika vituo vya chanjo kwa uhuru na usalama.
Video inaanzia katika Kituo cha Afya cha Al-Daraj kilichoko Gaza City, Palestina. Wazazi wanaume kwa wanawake wakiwa na watoto wao wamefurika kituoni hapo, wakihudumiwa na wahudumu wa afya kabla ya kupata chanjo.
Refqa Skaik, Afisa wa Kiufundi wa Polio katika WHO, anasema, “kwa ushirikiano na Wizara ya Afya, UNICEF, Jumuiya Mwezi Mwekundu ya Palestina na sisi WHO, tunatoa utaalamu na msaada wa kiufundi katika utekelezaji wa kampeni hii, hususan kwa kundi la watoto walio chini ya miaka mitatu, wanaokadiriwa kufikia watoto 44,900.”









image quote pre code