Hatua ya makundi tutatumia Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar,” amesema Kamwe

Hatua ya makundi tutatumia Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar,” amesema Kamwe

#1

Klabu ya Yanga SC imetangaza rasmi kuwa itacheza mechi zake zote tatu za nyumbani katika hatua ya makundi ya michuano ya kimataifa kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, visiwani Zanzibar.

Akizungumza kupitia taarifa rasmi ya klabu, Ofisa Habari wa Yanga SC, Ali Kamwe, amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya uongozi kufanya tathmini ya kina na kuangalia maslahi mapana ya klabu katika kipindi hiki muhimu.

“Baada ya uongozi kufanya tathimini na kuangalia maslahi mapana ya Klabu yetu, nipende kuwatangazia kuwa mechi zetu zote tatu za nyumbani kwenye hatua ya makundi tutatumia Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar,” amesema Kamwe.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code