Je,Unatakiwa kunywa maji kiasi gani kwa Usalama wa Figo Zako?

Je,Unatakiwa kunywa maji kiasi gani kwa Usalama wa Figo Zako?

#1

Fahamu Figo ni moja ya viungo muhimu vya mwili wa mwanadamu, ambavyo vina majukumu mengi ya kuweka mwili katika afya njema.

Madaktari mara nyingi wanashauri kwamba ili kuweka figo kuwa na afya njema, kula kiasi cha chumvi, kuepuka sukari ya ziada na kutotumia dawa za maumivu bila ushauri wa daktari.

Hatua nyingine nyingi pia zinapendekezwa ili kuepuka shinikizo nyingi kwenye figo.

Kwa hivyo ni muhimu kunywa kiasi fulani cha maji ili kuweka figo kuwa na afya? Katika ripoti hii, tutajaribu kupata majibu kwa maswali haya.

Figo hufanya kazi ili kudumisha usawa wa electrolyte katika mwili wetu. Inadhibiti kiasi cha vipengele kama sodiamu na potasiamu.

Dkt. Vivekanand Jha, rais wa zamani wa Jumuiya ya Kimataifa ya Nephrology na mkurugenzi mtendaji wa Taasisi ya George ya Afya ya duniani, ni mtaalamu wa magonjwa ya figo.

Anasema, "Figo huondoa vitu visivyo vya lazima kutoka kwa mwili, ambavyo tunavipata kupitia chakula au kwa njia zingine. Na pia vitu ambavyo hutengenezwa mwilini kimetaboliki."

Dkt. Vivekanand Jha anasema, "Figo pia huzalisha aina nyingi za homoni mwilini, ambazo ni pamoja na kutengeneza damu, homoni zinazodhibiti shinikizo la damu na homoni za kudumisha usawa wa elektroliti."

Mtu wa kawaida anahitaji lita tatu hadi tatu na nusu za maji kila siku. Si lazima kwamba kiasi hiki kinatimizwa tu na maji ya kawaida. Inaweza kutimizwa na aina yoyote ya kioevu. Ikiwa tunadumisha usawa wa maji katika mwili, basi uwezekano wa maambukizi ya mkojo pia hupungua."

"Kwa watu wanaougua ugonjwa wa moyo au figo, kiasi cha maji kinachotumiwa huzuiwa kidogo ili kisiwe na shinikizo kubwa kwa viungo hivyo."

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code