Serikali ya Uingereza imeelezea kwa mara ya kwanza jinsi inavyolenga kutimiza ahadi yake ya kuondoa tafiti na majaribio kupitia wanyama.
Mipango hiyo ni kupunguza matumizi ya mbwa na sokwe katika vipimo vya dawa za binadamu kwa angalau 35% ifikapo 2030.
Chama cha Labour kilisema katika manifesto yake kwamba "kitashirikiana na wanasayansi, viwanda, na mashirika ya kiraia kukomesha tafiti kupitia wanyama.''
Waziri wa Sayansi Lord Vallance aliambia BBC, ipo siku matumizi ya wanyama katika sayansi yatakomeshwa kabisa lakini anakubali kwamba itachukua muda.
Majaribio kupitia wanyama nchini Uingereza yalifikia milioni 4.14 mwaka 2015 kutokana na ongezeko kubwa la tafiti za urekebishaji jeni – hasa kwenye panya na samaki.
Kufikia 2020, idadi hiyo ilishuka kwa kasi hadi milioni 2.88 huku mbinu mbadala zikibuniwa.
Lord Vallance aliiambia BBC anataka kubadilisha majaribio ya wanyama ili kuwepo majaribio kupitia tishu za wanyama, AI, na kompyuta.
Kulingana na mipango ya serikali, ifikapo mwisho mwa 2025, wanasayansi wataacha kutumia wanyama kwa majaribio makubwa na kubadili njia mpya katika maabara zinazotumia seli za binadamu.









image quote pre code