Mwishoni mwa wiki hii, mtandao wa kijamii wa X umezindua kipengele kipya ambacho kinawaruhusu watumiaji kuona nchi au eneo ambalo mtumiaji wa akaunti yupo.
Kulingana na mkuu wa masoko wa X, Nikita Bier, akaunti rasmi za serikali hazitaonyesha maeneo zilipo "ili kuzuia vitendo vya kigaidi dhidi ya viongozi wa serikali.”
Kipengele hiki, kinachoitwa "kuhusu akaunti hii," kinaweza kuonekana katika wasifu wa mtumiaji yeyote na kubainisha nchi au eneo ambalo mara nyingi hutumia akaunti yake.
X imefafanua kuwa taarifa kuhusu mahali akaunti inapopatikana inaweza kuathiriwa na safari, kwa hivyo huenda maelezo yasiwe sahihi na yanaweza kubadilika mara kwa mara.









image quote pre code