Kuanzia tarehe 10 Desemba, kampuni za mitandao ya kijamii zitakuwa na wajibu wa kuchukua "hatua zinazofaa" kuhakikisha kwamba watoto wenye umri chini ya miaka 16 nchini Australia hawawezi kuanzisha akaunti kwenye majukwaa yao na kwamba akaunti zilizopo zifutwe au kuzimwa.
Serikali inasema marufuku hiyo, sera ya aina yake duniani iliyopendwa na wazazi wengi, inalenga kupunguza "shinikizo na hatari" ambazo watoto wanaweza kukabiliana nazo kwenye mitandao ya kijamii, zinazotokana na "vipengele vya muundo vinavyowahamasisha kutumia muda mwingi kwenye skrini, huku pia vikionesha maudhui yanayoweza kuharibu afya na ustawi wao."
Utafiti ulioagizwa na serikali mwanzoni mwa mwaka huu ulionesha kuwa asilimia 96 ya watoto wenye umri wa miaka 10-15 walitumia mitandao ya kijamii na kwamba saba kati ya kumi kati yao walikuwa wamethibitishwa kuathirika na maudhui na tabia hatarishi.
Tabia hizi zilijumuisha kutoka kwenye maudhui ya ubaguzi dhidi ya wanawake, video za mapigano, hadi maudhui yanayohimiza matatizo ya kula na kujiua.
Mtoto mmoja kati ya saba pia aliripoti kuathirika na tabia za ukandamizaji kutoka kwa watu wazima au watoto wakubwa, na zaidi ya nusu walisema kuwa walikuwa wahanga wa unyanyasaji mtandaoni (cyberbullying).
Serikali ya Australia hadi sasa imeorodhesha majukwaa kumi yatakayojumuishwa kwenye marufuku: Facebook, Instagram, Snapchat, Threads, TikTok, X, YouTube, Reddit na majukwaa ya mtiririko wa video ya Kick na Twitch.
Pia ipo chini ya shinikizo la kupanua marufuku hadi kwenye michezo ya mtandaoni.
Wakiwa na hofu ya kuwa wanaweza kuingizwa kwenye marufuku, majukwaa ya michezo kama Roblox na Discord hivi karibuni yameanzisha ukaguzi wa umri kwenye baadhi ya vipengele kwa lengo la kujaribu kuepuka kuingizwa kwenye marufuku hiyo.
Serikali imesema itaendelea kukagua orodha ya majukwaa yaliyoathirika, na itazingatia vigezo vikuu vitatu wakati wa kufanya hivyo.









image quote pre code