Papa Leo alisema ni kashfa kwamba Wakristo bilioni 2.6 duniani hawana umoja thabiti

Papa Leo alisema ni kashfa kwamba Wakristo bilioni 2.6 duniani hawana umoja thabiti

#1

Katika sherehe za maadhimisho ya miaka 1,700 ya baraza kuu la Kanisa lenye makasisi wakuu kutoka nchi zikiwemo Uturuki, Misri, Syria na Israel, zilizoandaliwa mjini Iznik ambao awali ulijulikana kama Nicaea, Papa Leo alisema ni kashfa kwamba Wakristo bilioni 2.6 duniani hawana umoja thabiti.

Kiongozi huyo wa kanisa Katoliki pia amesema kwasasa, ubinadamu wote ulioathirika kwa vurugu na mizozo unataka maridhiano na upatanisho.

Pia amesema lazima watu wapinge matumizi ya dini kuhalalisha vita, vurugu ama mfumo wowote wa kiitikadi na kuongeza kusema njia za kufuata ni mazungumzo na ushirikiano.

Consultation ya Afya Moja kwa Moja

Mimi ni Dr. Ombeni Mkumbwa. Nakupa ushauri wa kitaalamu kuhusu tatizo lolote la kiafya kwa siri, haraka na uhakika.

WhatsApp

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code