Rais aagiza kuhamishwa kwa polisi wanaolinda watu mashuhuri Nigeria

Rais aagiza kuhamishwa kwa polisi wanaolinda watu mashuhuri Nigeria

#1

Rais wa Nigeria ameagiza kuhamishwa kwa maafisa wa polisi wanaolinda watu mashuhuri hadi sehemu zingine kukabiliana na tatizo la usalama nchini humo.

Rais Bola Ahmed Tinubu ameamuru kuhamishwa kwa maafisa hao baada ya wanafunzi 50 kati ya zaidi ya 300 waliotekwa nyara kutoka shule ya Katoliki huko Nigeria kufanikiwa kutoroka kutoka kwa watekaji wao.

Tinubu alikaribisha habari hiyo, na kuongeza kwamba alikuwa akielezewa juu ya hali ya usalama kote nchini.

Operesheni ya utafutaji na uokoaji inaendelea kwa wanafunzi na walimu ambao walitekwa nyara na watu wenye silaha siku ya Ijumaa.

Shule katika eneo hilo la Nigeria zimeamriwa kufungwa.

Kuongezeka kwa matukio ya utekaji nyara wa watu wengi hivi karibuni kunatokea wakati utawala wa Trump umekosoa viongozi wa Nigeria kwa kushindwa kuwalinda Wakristo kutokana na kuuawa na wanamgambo wa Kiisilamu, madai ambayo serikali imekanusha.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code