Serikali ya Israel imethibitisha kuwa mwili wa marehemu Joshua Luito Mollel, mwanafunzi kutoka Tanzania aliyechukuliwa mateka katika Ukanda wa Gaza tarehe 7 Oktoba 2023, umetambuliwa rasmi.
Utambulisho huo umefanywa na Kituo cha Kitaifa cha Tiba ya Uchunguzi wa Vifo kwa ushirikiano na Polisi ya Israel na Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF).
Familia ya marehemu imejulishwa rasmi, na mwili wake umerejeshwa nchini Israel.
Serikali ya Israel imetoa salamu za rambirambi kwa familia ya Mulal na kwa familia zote za mateka waliopoteza maisha.
Serikali na Jeshi la Ulinzi la Israel wamesisitiza kuwa wanaendelea kufanya kila juhudi kuhakikisha kuwa miili ya mateka wote inarejeshwa kwa maziko yenye heshima.
Vilevile, serikali imeitaka Hamas kutekeleza makubaliano na kurejesha miili ya mateka waliobaki.
Wamesema hawatapumzika hadi kila mmoja arejeshwe nyumbani. via Bbc.









image quote pre code