Usugu wa vimelea dhidi ya dawa (Uvida) changamoto hatari Zaidi

Usugu wa vimelea dhidi ya dawa (Uvida) changamoto hatari Zaidi

#1

Usugu wa vimelea dhidi ya dawa (Uvida) changamoto inayofanya maradhi ya kawaida kuwa hatari kubwa inayotishia maisha, kimya kimya.

Kwa mujibu wa Kituo cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa Afrika (Africa CDC), Uvida hutokea pale dawa zinazotumika kuua vimelea vya ugonjwa zinaposhindwa kufanya kazi kutokana na vimelea kuwa sugu dhidi ya nguvu ya dawa hizo. 

Shirika la Afya Duniani (WHO) linakadiria kuwa Uvida unasababisha vifo vya moja kwa moja zaidi ya milioni 1.3 duniani huku ikichangia vifo milioni 5 kila mwaka.

Mbali na athari za kiafya, tatizo hili linatishia pia uchumi wa dunia ambapo inakadiriwa kuwa ifikapo mwaka 2030, gharama za tatizo hili kimataifa zinatarajiwa kufikia hadi Dola  za Marekani trilioni 3.4 (sawa na takriban Sh9,860 trilioni).

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code