Mamlaka ya Taliban nchini Afghanistan imewaamuru wagonjwa wa kike, walezi na wafanyakazi kuvaa burka - vazi kamili la Kiislamu - ili kuingia katika vituo vya afya vya umma katika mji wa magharibi wa Herat, shirika la matibabu la Médecins Sans Frontières (MSF) linasema.
MSF ilisema vikwazo hivyo vilianza kutekelezwa kuanzia tarehe 5 Novemba.
"Vikwazo hivi vinatatiza zaidi maisha ya wanawake na kuwazuia kupata huduma za afya," Sarah Chateau, meneja wa programu wa shirika hilo nchini Afghanistan, aliiambia BBC. Alisema hata wale "wanaohitaji huduma ya haraka ya matibabu" wameathirika.
Msemaji wa serikali ya Taliban amekanusha madai ya MSF. Ripoti zinasema vizuizi vimelegezwa kwa kiasi tangu kuanza kuangaziwa kwa suala hilo.









image quote pre code