Anthony Albanese,Waziri Mkuu wa kwanza aliye madarakani katika historia ya Australia kufunga ndoa

Anthony Albanese,Waziri Mkuu wa kwanza aliye madarakani katika historia ya Australia kufunga ndoa

#1

Waziri Mkuu wa Australia Anthony Albanese amefunga ndoa rasmi na mwenzi wake, Jodie Haydon — akiwa Waziri Mkuu wa kwanza aliye madarakani katika historia ya nchi hiyo kufunga ndoa wakiwa ofisini.

Wawili hao walikula kiapo Jumamosi alasiri ndani ya The Lodge, makazi yake rasmi huko Canberra, siku moja tu baada ya bunge kukamilisha kikao chake cha mwisho cha mwaka huo, BBC iliripoti.

Harusi hiyo ilifichwa kwa sababu za kiusalama, huku wanafamilia wa karibu na mawaziri wakuu pekee wakihudhuria. Wazazi wa Jodie Haydon, pamoja na mtoto wa kiume wa Albanese, Nathan, walikuwepo kushuhudia sherehe hiyo.

if you want to request theme or script please, Read Here!
Please Disable the AdBlock or add our website in Whitelist to Support NiaDZGN
Read Here! NiaDZGN Terms and Rules

image quote pre code