Gharama za Smartphone kuongezeka zaidi 2026,Kisa AI

Gharama za Smartphone kuongezeka zaidi 2026,Kisa AI

#1

Dunia inaenda kushuhudia ongezeko maradufu la mauzo ya simu janja kuanzia mwaka 2026 tofauti na ilivyo kawaida, na hii ni kwa sababu ya ongezeko la gharama ya uzalishaji wa chipset zinazoendesha simu janja. 

Mabadiliko ya teknolojia ya leo yanayotegemea uendeshaji wa mifumo ya AI, unahitaji chip zenye uwezo wa kufikiri na kuchakata data kwa kasi ya juu. 

Taarifa ya jarida la BUSINESS WORLD inaeleza kuwa dunia inaelekea zama mpya za “super smartphones,” ambazo zitakua na uwezo mkubwa maradufu zaidi tofauti za simu janja za zamani, na mabadiliko haya yanahitaji uwekezaji kwenye chipset zinazoendesha simu janja zote duniani.

Kampuni kubwa za utengenezaji chipset duniani zimeanza kuuza chipset hizi kwa bei ya ongezeko la 10% jambo litakalowalazimu kampuni za simu duniani kupandisha gharama za mauzo ya simu ili kumudu gharama mpya za utengenezaji wa simu janja zao.

Umejipangaje kununua simu janja mpya mwaka 2026?

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code