Marufuku ya mitandao ya kijamii kwa vijana chini ya miaka 16 yaanza kutekelezwa Australia

Marufuku ya mitandao ya kijamii kwa vijana chini ya miaka 16 yaanza kutekelezwa Australia

#1

Australia imekuwa nchi ya kwanza duniani kupiga marufuku ufikiaji wa mitandao ya kijamii kwa watoto walio chini ya umri wa miaka 16, hatua iliyopokelewa vyema na wazazi wengi na watetezi wa haki za watoto lakini ikikosolewa na makampuni ya teknolojia na watetezi wa uhuru wa kujieleza.

"Ni siku ya kujivunia kuwa waziri mkuu wa Australia," anasema Anthony Albanese wakati marufuku ya akaunti za mitandao ya kijamii kwa walio chini ya miaka 16 inaanza kutekelezwa kwa mara ya kwanza duniani.

Miongoni mwa majukwaa yanayohitajika kutekeleza sheria hii mpya ni Pamoja na Instagram, Facebook, Threads, X, Snapchat, Kick, Twitch, TikTok, Reddit na YouTube.

Lulu mwenye umri wa miaka 15 ameionesha BBC jinsi akaunti zake zilivyogoma kufunguka muda mfupi baada ya kuanza kutekelezwa kwa hatua hiyo.

“Nilikuwa na hasira sasa ninajitahidi kuzoea hali hii ninasikia huzuni”binti mwingine alieleza

Serikali inasema marufuku hiyo inalenga kuwalinda vijana kutokana na maudhui hatarishi, lakini wakosoaji wanapendekeza kwamba inaweza kuwatenga vijana walio katika mazingira magumu na kuwasukuma watoto kwenye maeneo yasiyodhibitiwa za mtandao.

Serikali inasema marufuku hiyo inalenga kuwalinda vijana kutokana na maudhui hatarishi, lakini wakosoaji wanapendekeza kwamba inaweza kuwatenga vijana walio katika mazingira magumu na kuwasukuma watoto kwenye maeneo yasiyodhibitiwa kwa njia za kimtandao.

“Hii ni hatua ya kijasiri ambayo nchi zingine nyingi zinaiangalia kwa makini lakini bado haijafahamika kwa namna gani serikali itapima mafanikio yake”, anaandika mwandishi wa BBC Australia.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code