Mwanaume mmoja kutoka Nigeria asherehekea mkewe kuzaa mapacha baada ya miaka 16 ya kusubiri
Mwanamume wa Nigeria, Collins Egwurugwu, amesherehekea kuwa baba baada ya miaka 16 ya ndoa.
Alitumia Facebook siku ya Jumapili, Novemba 30, 2025 kutangaza kwamba mkewe amezaa mapacha wa kiume.
Watoto hao walizaliwa Jumamosi, Novemba 29.
Akikumbuka miaka ya kusubiri, maumivu, machozi na kumuuliza Mungu maswali, Collins alikiri kuwa haikuwa uamuzi rahisi kushikilia tumaini hilo.
Aliongeza kuwa mengi yalimjia akilini lakini hakutaka kufuata nyayo za baba yake.









image quote pre code