Sri Lanka:Kimbunga Ditwah chaacha uharibifu mkubwa na kuua watu 159

Sri Lanka:Kimbunga Ditwah chaacha uharibifu mkubwa na kuua watu 159

#1

Mamlaka nchini Sri Lanka zinapambana na mafuriko yanayoongezeka katika maeneo ya mji mkuu Colombo, baada ya Kimbunga Ditwah kuacha uharibifu mkubwa na kuua watu 159 kote nchini.

Zaidi ya watu 203 bado hawajulikani walipo, huku mvua kubwa ikisababisha maji ya Mto Kelani kufurika. Rais Anura Kumara Dissanayake ametangaza hali ya dharura na kuomba msaada wa kimataifa.

India imetuma misaada na helikopta mbili kwa operesheni za uokoaji, huku Japan ikiahidi msaada zaidi. Zaidi ya nyumba 20,000 zimeharibiwa, na watu 122,000 wamehifadhiwa kwenye kambi za muda.

Zaidi ya watu laki nane wanahitaji msaada, na karibu theluthi moja ya nchi haina umeme na maji safi. Kimbunga Ditwah kimekuwa janga baya zaidi nchini humo tangu mwaka 2017.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code