Wagonjwa wa Malaria waliongezeka duniani 2024,WHO

Wagonjwa wa Malaria waliongezeka duniani 2024,WHO

#1

Shirika la Afya Duniani, WHO limesema ugonjwa wa malaria uliwaua takribani watu 610,000 duniani kote mwaka 2024.


Ripoti ya mwaka ya WHO kuhusu malaria iliyotolewa Alhamisi, imeeleza kuwa visa vya ugonjwa huo vimeongezeka zaidi nchini Ethiopia, Madagascar na Yemen.

Idadi hiyo ni juu kidogo ikilinganishwa na vifo vya 2023, huku maambukizi mapya yakipanda kutoka milioni 273 hadi takribani milioni 282.

Baada ya hatua kubwa kupigwa mwanzoni mwa miaka ya 2000, mapambano dhidi ya malaria yamekuwa yakisuasua katika muongo mmoja uliopita.

Nchi kadhaa hazina malaria

Hata hivyo, nchi 47 zimethibitishwa kutokuwa na malaria.

Daniel Ngamije Madandi, Mkurugenzi wa Mpango wa Kimataifa wa Kupambana na Malaria wa WHO, amesema watu wengi bado wanapoteza maisha kutokana na ugonjwa ambao unaweza kuzuilika na kutibika.

WHO imesema kuongezeka kwa maambukizi kunachangiwa na ongezeko la dawa zisizo na ubora wa kutibu malaria, mabadiliko ya tabianchi na kupungua kwa ufadhili.

Changia Mada hapa(Reply)


image quote pre code